





























Hadeeth Cards
Da'wa cards that highlight great meanings from the noble prophetic hadiths in a simple style and attractive display that helps the Muslim to have a deeper understanding of his religion in an easy way
All
Imepokelewa kutoka kwa Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: Kuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa anapolala kitandani kwake wakati wa kila usiku alikuwa akikusanya viganja vyake, kisha akivipuliza na kuvisomea : {Qul-huwallahu Ahad}, na {Qul-A uudhu birabbil falaq} na (Qul-Auudhu birabbi naas } Kisha hujipaka kwa viganja hivyo sehemu awezayo katika mwili wake, anaanza kupaka kichwa chake na uso wake na sehemu ya mbele ya mwili wake, anafanya hivyo mara tatu.
Imepokelewa na Al-BukhaariyIlikuwa katika miongozo yake Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- pindi anapopanda kitandani kwake kwa ajili ya kulala, ni kukusanya viganja vyake na kuviinua juu kama anavyofanya mwenye kuomba-na huvipuliza viganja hivyo kwa mdomo wake upulizaji wa taratibu pamoja na kutemea matemate kidogo na anasoma Sura tatu {Qul-huwallahu Ahadu} na {Qul-audhu birabbil falaq} na {Qul-auudhu birabbi naas} Kisha hupaka kwa kutumia viganja vyake sehemu anayoweza katika mwili wake; Kwa kuanzia kichwa chake na uso wake na sehemu ya mbele katika mwili wake, na hurudia kitendo hicho mara tatu.
Kutoka kwa Adiy bin Hatim kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Mayahudi wameghadhibikiwa, na Wakristo ni wapotofu".
Imepokelewa na Imamu TirmidhiyAmeeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- yakuwa Mayahudi ni watu waliokasirikiwa na Mwenyezi Mungu; kwa sababu waliujua ukweli na wala hawakuufanyia kazi. Na Wakristo ni watu waliopotea; kwa sababu walifanya matendo bila ya elimu.
Imepokelewa kutoka kwa Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Alisoma Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake Aya hii :{Yeye ndiye ambaye alikuteremshia kitabu hiki ndani yake kuna Aya muhkam -zilizo wazi- aya hizo ambazo ndiyo msingi wa kitabu hiki na zipo nyingine zinatatiza, wale ambao nyoyoni mwao kuna upotofu watafuata zile zenye kutatiza kwa kutaka kufitinisha na kutaka kujua uhakika wa maana yake, na hakuna ajuaye uhakika wa maana yake isipokuwa Mwenyezi Mungu, na wale wabobezi katika elimu wanasema tumeziamini zote zimetoka kwa Mola wetu na hawakumbuki isipokuwa wenye akili} (Al- imaraan 7) Anasema Aisha: Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake akasema: "Ikiwa utawaona wenye kufuata Aya zenye kutatiza basi hao ndiyo ambao Mwenyezi Mungu amewataja katika aya"
Wamekubaliana Bukhaariy na MuslimMtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alisoma aya hii: {Huwal ladhii Anzala alaikal kitaab minhu aayaatu muhkamaatun hunnaa ummul kitaab,wa ukharu mutashaabihaat,fa-ammal ladhiina fii quluubihim zaighun fayattabiuuna maatashaabaha minhu ib-tighaal fitnat wabtighaa taawiilihi,wamaa yaalamu taawilahu illa llahu warrasikhuuna fil ilmi yaquuluuna aamanna bihi kullu min in-di rabbinaa wamaa yaddhakkaru illa ulul al-baab}, Ndani ya aya hii Mwenyezi Mungu Mtukufu amefahamisha kuwa yeye ndiye aliyeteremsha Qur'ani kwa Mtume wake Qur'ani ambayo kuna aya zinazofahamika kwa uwazi, hukumu zake zinafahamika na hazitatizi, na aya hizo ni msingi wa kitabu hiki na ndiyo marejeo yake, nayo Qur'ani ndiyo marejeo inapotokea kutofautiana, na katika Qur'ani hiyo kuna aya zingine zinachukuwa maana zaidi ya moja maana zake zinawatatiza baadhi ya watu, au wanadhani kuwa kati ya aya na aya nyingine kuna mgongano, kisha akaweka wazi Mwenyezi Mungu namna watu wanavyozifanyia kazi aya hizi, basi wale ambao katika nyoyo zao kuna upotofu wa kuiwacha haki huziwacha aya zilizokuwa wazi, na wanachukuwa zile zenye kutatiza wakitaka kuibua utata na kuwatatiza watu, na kufanya hivyo wanataka kwa kutumia maana hiyo iafikiane na matamanio ya nafsi zao, ama wale ambao wamebobea kwenye elimu wanaujua utata huu, na wanazirudisha kwenye maana zilizo wazi na wanaziamini kuwa aya hizo zimetoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na haiwezekani zikapingana lakini hilo hawalikumbuki wala kupata mawaidha isipokuwa wale wenye akili iliyo salama, kisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akamwambia mama wa waumini Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa ikiwa atawaona wenye kufuata aya zenye kutatiza basi hao ndio wale ambao Mwenyezi Mungu amewataja katika maneno yake aliposema: {Basi wale ambao katika nyoyo zao kuna maradhi} basi tahadhari nao na wala usiwasikilize.
Imepokelewa kutoka kwa Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: Ya kuwa mtu mmoja alikaa mbele ya Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, kwa hakika mimi nina watu niliowamiliki, wakati mwingine wananidanganya na wananifanyia hiyana na wanakwenda kinyume na amri zangu, nahuwa nawatia adabu kwa kuwatukana na kuwapiga, hivyo naulizia kuwa ni vipi itakuwa hali yangu kwa kuwafanyia hayo?Akasema: "Watahesabiwa kwa hiyana waliyokufanyia na kukuasi na kukudanganya, na itahesabiwa adhabu yako uliyowapa basi ikiwa adhabu uliyowapa ipo sawa na makosa yao basi itatosha na hapatakuwa na chochote kwako wala kwao, na ikiwa adhabu uliyowapa ni ya chini kulingana na kosa walilofanya basi utalipwa na utazidishiwa kwenye malipo yako, na ikiwa umewaadhibu zaidi ya walivyokosea yatapunguzwa kutoka kwako malipo ya ziada" Akasema: Basi yule bwana alijitenga na akawa analia kwa sauti ya juu, Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akamwambia: "Hivi husomi katika kitabu cha Mwenyezi Mungu aliposema: "Na Sisi tutaweka Mizani ya uadilifu siku ya Kiyama na hakuna nafsi yoyote itakayodhulumiwa kwa chochote", mpaka mwisho wa Aya, yule bwana akasema: Nakuapia ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, sijaona kheri iliyopo kati yangu na yao zaidi ya kuwaachia huru, na ninakupa ushuhuda kuwa wao wote kuanzia sasa wako huru".
Imepokelewa na Imamu TirmidhiyAlikuja mtu mmoja kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akishitakia kuhusu matendo ya Watumwa wake, Watumwa hao wanamdanganya na kumfanyia hiyana katika amana, na wanafanya ghushi katika miamala, na wanakwenda kinyume na maelekezo yake, naye huwatia adabu kwa kuwatukana na kuwapiga, hivyo akaulizia kuhusu hali yake itakavyokuwa siku ya Kiyama, basi Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akasema: Watahesabiwa kwa kile walichokufanyia hiyana na kwenda kinyume na maelekezo yako na kukudanganya na wewe utahesabiwa ulivyo waadhibu, basi ikiwa adhabu uliyowapa itakuwa sawa na makosa yao basi hutokuwa na kosa lolote, na ikiwa adhabu uliyowapa ni ndogo ikilinganishwa na kosa walilofanya basi ni jambo zuri utalipwa na utazidishiwa katika malipo yako, na ikiwa adhabu uliyowapa ni zaidi ya walichokifanya, basi utaadhibiwa na malipo yako uliyozidishiwa yatachukuliwa na watapewa wao, basi yule bwana akakaa pembeni akawa analia kwa sauti ya juu, Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akamwambia: "Hivi husomi katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu aliposema: "Na Sisi tutaweka Mizani ya uadilifu siku ya Kiyama na hakuna nafsi yoyote itakayodhulumiwa kwa chochote, hata kama jambo hilo litakuwa na uzito sawa na punje ya Hardal tutalileta Nasi tunatosha kuwa wajuzi wa hisabu" (Al-Anbiyaa 47), hivyo basi hatodhulumiwa mtu yoyote siku ya kiyama, na kipimo cha watu kitakuwa cha uadilifu, yule bwana akasema: Nakuapia ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, sijaona kheri iliyopo kati yangu na wao zaidi ya kuwaacha huru ninakupa ushuhuda kuwa wao wote kuanzia hivi sasa wako huru kwa ajili ya Mwenyezi Mungu; kwa kuogopea hesabu na adhabu.
Imepokewa kutoka kwa bin Abbas -Radhi za Allah ziwe juu yao yeye na baba yake-: Yakwamba watu miongoni mwa washirikina walikuwa wameuwa watu, na wakakithirisha mauaji, na wakazini na wakikithirisha zinaa, wakamjia Muhammadi -Rehema na amani ziwe juu yake- wakasema: Hakika haya unayoyasema na kuwalingania watu ni mambo mazuri, ikiwa utatwambia juu ya haya tuliyoyafanya kama yana kafara, ikateremka kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na wale ambao hawamuombi pamoja na Mwenyezi Mungu mungu mwingine na wala hawauwi nafsi aliyoiharamisha Mwenyezi Mungu isipokuwa kwa haki na wala hawazini" [Al-Furqan: 68], na ikateremka: "Sema: Enyi waja wangu waliojidhulumu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu..." [Az-Zumar: 53].
Wamekubaliana Bukhaariy na MuslimWalikuja watu miongoni mwa washirikina kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- na walikuwa wamekwisha fanya mauaji mengi na zinaa nyingi, wakasema kumwambia Mtume: Hakika Uislamu unaoulingania na mafundisho yake ni mazuri, lakini sisi tutakuwa na hali gani kwa yale tuliyoyatenda miongoni mwa ushirikina na madhambi makubwa, je, yanakafara?. Zikateremka aya mbili, kiasi ambacho Mwenyezi Mungu aliwakubalia watu toba zao pamoja na wingi wa madhambi yao na ukubwa wake, na lau kama si hivyo basi wangeendelea kubaki katika ukafiri wao na ujeuri wao wala wasingeingia katika dini hii.
Na kutoka kwa Ibn Omari Radhi za Allah ziwe juu yake na baba yake: Ya kwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- aliwahutubia watu siku ya ufunguzi wa mji wa Makka, akasema: "Enyi watu hakika Mwenyezi Mungu ameondosha kwenu nyinyi kiburi cha zama za ujinga, na kujifaharisha kwa nasaba , basi watu wako aina mbili: Mwema mchamungu mtukufu kwa Mwenyezi Mungu, na muovu mbaya dhalili kwa Mwenyezi Mungu, na watu wote ni wana wa Adam, na amemuumba Mwenyezi Mungu Adam kutokana na udongo. Amesema Mwenyezi Mungu: "Enyi watu hakika sisi tumekuumbeni kutokana na mwanaume na mwanamke na tukakufanyeni kuwa mataifa na makabila tofauti tofauti, ili mfahamiane, hakika mbora wenu kwa Mwenyezi Mungu ni mchamungu wenu, hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi na ana habari (za mambo yote)" [Al Hujuraat: 13].
Imepokelewa na Imamu TirmidhiyAliwahutubia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- watu siku ya ufunguzi wa mji wa Makka akasema: Enyi watu! Hakika Mwenyezi Mungu amenyanyua na akaondosha kwenu nyinyi kiburi cha zama za ujinga na kujiona, na kujifaharisha kwa baba zenu (nasaba), bali watu wako aina mbili: Ni ima muumini mwema, mchamungu, mtiifu, mwenye kumuabudu Mwenyezi Mungu Mtukufu, huyu ni mtukufu mbele ya Mwenyezi Mungu, hata kama hana cheo au nasaba nzuri mbele za watu. Na ima kafiri muovu, na huyu ni dhalili kwa Mwenyezi Mungu, na wala hana thamani yoyote, hata kama ana ukoo mzuri na cheo na mamlaka. Na watu wote ni watoto wa Adam, na Mwenyezi Mungu kamuumba Adam kutokana na udongo, haifai kwa kiumbe ambaye asili yake ni udongo kuwa na kiburi na kujiona yeye ni bora, na hili linasadikishwa na kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Enyi watu! hakika sisi tumekuumbeni nyinyi kutokana na mwanaume na mwanamke na tukakufanyeni kuwa mataifa na makabila ili mpate kujuana, hakika mbora wenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni mchamungu wenu, hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi na ana habari (ya myafanyayo) [Alhujrat:13].
Kutoka kwa Zubairi bin Awwam amesema: Ilipoteremka: "Kisha hakika bila shaka mtakuja kuulizwa kuhusu neema" [Takathur: 8], akasema Zubairi: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ni neema zipi tutakazooulizwa juu yake, au ni hivi vyeusi viwili tende na maji (Vyakula na vinywaji kwa ujumla)? Akasema: "Hakika bila shaka zitakuwa hizo".
Imepokelewa na Imamu TirmidhiyIlipoteremka aya: "Kisha hakika bila shaka mtaulizwa siku hiyo kuhusu neema" Yaani: Mtakuja kuulizwa kuhusu kutekeleza shukurani kwa yale aliyowaneemesha Mwenyezi Mungu juu yenu miongoni mwa neema, akasema Zubairi bin Awwam radhi za Allah ziwe juu yake: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ni neema zipi tutakazoulizwa juu yake?! Ni neema mbili ambazo hazihitaji kuziomba ambazo ni tende na maji!. Akasema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-: Ama hakika nyinyi mtaulizwa kuhusu neema pamoja hali hii iliyo nayo, ni hizi neema mbili kubwa katika neema za Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Imepokewa Kutoka kwa Abuu Mussa Al-Ash'ary-Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Shikamaneni vizuri na hii Qur'ani, namuapa yule ambaye nafsi ya Muhammadi iko mkononi mwake, hutoroka kwa kasi mno kuliko hata Ngamia katika kamba yake".
Wamekubaliana Bukhaariy na MuslimAmeamrisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kushikamana na Qur'ani na kudumu na kuisoma ili mtu asiisahau baada yakuwa kaihifadhi katika kifua chake, na akalisisitiza hilo kwa kiapo chake -Rehema na amani ziwe juu yake- yakwamba Qur'ani hujitoa haraka mno na kuondoka kutoka vifuani kuliko hata Ngamia aliyefungwa, naye ni yule aliyekazwa kwa kamba kati kati ya muhundi, mtu akikaa karibu naye atamshika, na akimuacha ataondoka na atapotea.
Imepokewa kutoka kwa Othman -Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Mmbora wenu ni yule aliyejifunza Qur'ani na akaifundisha".
Imepokelewa na Al-BukhaariyAnaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- yakuwa muislamu bora na aliye na daraja ya juu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu: Ni yule aliyejifunza Qur'ani, kwa kuisoma na kuihifadhi na kuisoma vizuri na kuielewa na kuitafsiri, na akamfundisha mwingine kile alichonacho katika elimu za Qur'ani pamoja na kuifanyia kazi.